Maana: Kutoa humnufaisha anayepokea na anayetoa.
Methali 19:17: “Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, naye Atamlipa kwa anayotenda.”
Maana: Mungu anaona kwamba ana deni kwa wale wanaowasaidia wenye uhitaji, na anaahidi kuwalipa kwa ukarimu wao.
Mathayo 6:2: “Unapotoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki . . . ili wasifiwe na watu.”
Maana: Hatupaswi kutoa ili watu watutambue.
Matendo 20:35: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”
Maana: Ukarimu unaotoka moyoni huleta furaha.
2 Wakorintho 9:7: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.”
Maana: Kutoa kwa hiari humfurahisha Mungu.
0 Comments