MAANDIKO MATAKATIFU YANAYOHUSU KUTOA



Habari ndugu mpenzi msomaji wa Makala zetu kutoka hapahapa wilnismstore, leo nimekuandalia Makala fupi inayohusiana na Maandiko matakatifu yanayohusu kutoa, soma kwa umakini kisha kutafakari

Methali 11:25: “Mtu mkarimu atapata ufanisi, na yule anayewaburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa.”


Maana: Kutoa humnufaisha anayepokea na anayetoa.

Methali 19:17: “Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, naye Atamlipa kwa anayotenda.”

Maana: Mungu anaona kwamba ana deni kwa wale wanaowasaidia wenye uhitaji, na anaahidi kuwalipa kwa ukarimu wao.

Mathayo 6:2: “Unapotoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki . . . ili wasifiwe na watu.”

Maana: Hatupaswi kutoa ili watu watutambue.

Matendo 20:35: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”

Maana: Ukarimu unaotoka moyoni huleta furaha.

2 Wakorintho 9:7: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.”

Maana: Kutoa kwa hiari humfurahisha Mungu.

Amina na ubarikiwe,
Naamini mpaka hapa umeshajifunza kitu, niandikie maoni yako katika sehemu ya comments hapa chini

Post a Comment

0 Comments